Tetesi za Usajili Bongo
Habari za michezo

YANGA KUKIPIGA DODOMA DHIDI YA TABORA

Staff Desk December 20, 2023 1:03 pm

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imefanya mabadiliko ya uwanja wa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Tabora United dhidi ya Yanga SC

Mchezo huo namba 110, ambao timu Yanga SC itakuwa ugenini, sasa utachezwa Desemba 23, 2023, saa 1:00 Usiku kwenye Uwanja wa Jamhuri uliopo Dodoma.

Awali mchezo huo ulipangwa kuchezwa Desemba 22, 2023, saa 10:00 jioni kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi uliopo mkoani Tabora.

Kwa mujibu wa TPLB, sababu za mabadilko hayo ni Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi kufungiwa na Kamati ya Leseni za Klabu ya TFF.

MTIBWA NAE KAPATA PA KUFUFUKIA PHIRI AJIKUTA NJE YA LIST…. ISHU NZIMA IKO HIVI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply