Habari za Simba leo
Habari za michezo

BAADA YA KUANZA BALAA LAKE NA SIMBA….KICHUYA KAIBUKA NA HILI KWA CHASAMBI…

admin February 1, 2024 12:43 pm

Kiungo Mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Shiza Ramadhan ‘Kichuya’ amemng’ata sikio winga mpya wa timu hiyo, Ladack Chasambi kuwa kama anataka kufika mbali basi anapaswa kuwasikiliza nyota wazoefu aliowakuta watamfundisha vingi.

Amesema kuwa kinda huyo ameingia Simba SC ameikuta timu ikiwa imekamilika hivyo anatakiwa kupambana kwani tofauti na yeye wakati anatua mitaa ya Msimbazi walikuwa wanajitafuta.

“Simba SC iko tayari sio kama ile waliyokuwa wanaunga unga, Ladack ni mchezaji mzuri atulize akili ajue nini anatakiwa kufanya na wanasimba wanahitaji nini kutoka kwake atafika anapotakiwa kufika.

Lakini asiweke presha kubwa maana bado ni kijana mdogo ameenda kwenye timu kubwa umri wake na alipoenda ni vitu viwili tofauti, anatakiwa kupambana zaidi ya alipotoka,” amesema Kichuya

Amesema asijipe ukubwa anatakiwa ajue yeye bado ni mdogo anatakiwa kujifunza afanye kazi kwani miongoni mwa vijana ambao Mkoa wa Morogoro wanajivunia nao ni yeye na wanaamini kwa kipaji alichonacho ataisaidia Simba SC.

MASHINE YA KAZI ILIYOINGIA KWENYE ANGA ZA YANGA YAPAA ULAYA…JAMAA NI FUNDI NA NUSU.. PAMOJA NA KUSAMEHEWA…BENCHIKHA AMKUNJIA KIAINA CHAMA….ABAKISHWA DAR…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply