Habari za Simba leo
Habari za michezo

KUELEKEA MECHI NA AL AHLY….CHAMA AVUNJA UKIMYA SIMBA….ATAJA MTITI ULIOPO NDANI…

admin March 18, 2024 11:54 am

KIUNGO wa Simba, Clatous Chama amekiri kuwa mechi yao dhidi ya Al Ahly katika hatua ya robo fainali, itakuwa ngumu, lakini sasa ni muda wao wa kuandikia historia katika michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Simba inatarajiwa kuanza nyumbani katika mchezo wa robo fainali ya michuano hiyo dhidi ya Al Ahly ya Misri unaotarajiwa kuchezwa Machi 29, mwaka huu, uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam.

Chama amesema itakuwa mechi ngumu kwa kuwa wanafahamu ubora wa Al Ahly, watacheza kwa kuwaheshimu kwa sababu wanahitaji kufanya vizuri kuandika historia kwa mwaka huu.

Amesema malengo yao makubwa ni kupambana kuhakikisha wanafanya vizuri katika mchezo ujao dhidi ya Al Ahly kupata matokeo nyumbani, benchi la ufundi litafanyia kazi makosa yaliyojitokeza katika michezo iliyopita kwa ajili ya kufanya vizuri na kufikia malengo ya kuvuka robo fainali.

“Malengo yetu ni kuona tunavuka robo fainali kwa misimu minne tunaishia hatua hii, Al Ahly sio wageni kwetu tumekutana nao mara nyingi timu nzuri na bora lakini hatuwaogopi tunawaheshimuna tuko tayari kupambana,” amesema kiungo huyo aliyeenda kwao kwa ajili ya majukumu ya timu ya Taifa.

Ameongeza kuwa anaimani benchi la ufundi litafanyia kazi makosa yaliyojitokeza na kujiandaa kwa ajili ya ya mchezo huo, wachezaji wote wanatambua umuhimu wa mechi hiyo na hawana ugeni na Al Ahly kwa kuwa walikutana nao Tanzania na hata Misri.

FT:- AZAM FC 2-1 YANGA…..MGOLI WA FEI TOTO WAZUI JAMBO JANGWANI….MJI WOTE KIMYAAA… UTAJIRI WA SAMATTA NI KUFRU TUPU AISEEE…..JAMA ANAZAIDI YA BIL 40 BANK….MSHAHARA WAKE BALAA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply