Home Habari za Simba Leo SIMBA YAPIGA HODI KWA FEI TOTO…AZAM FC YATAJA BEI

SIMBA YAPIGA HODI KWA FEI TOTO…AZAM FC YATAJA BEI

Fei Toto, Habari za Simba

SIMBA na Mamelodi Sundowns zimeulizia uwezekano wa kumsainisha mkataba staa wa Azam FC, Feisal Salum ‘Fei Toto’ lakini zikaambiwa hauzwi.

Fei Toto ambaye alitua Azam FC akitokea Yanga, alisaini mkataba wa miaka mitatu na tayari ameutumikia kwa msimu mmoja akiisaidia timu hiyo kumaliza katika nafasi ya pili na kupata nafasi ya kuiwakilisha Tanzania katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

Uongozi wa Simba umeulizia uwezekano wa kumsajili mchezaji huyo ambaye inaelezwa kuwa thamani yake kwa sasa sokoni, ni  takribani Bilioni 1.5.

Awali miamba ya  Afrika Kusini Mamelod Sundowns walijaribu kuulizia saini ya mchezaji huyo, lakini hadi sasa bado hawajakuwa na msukumo mkubwa kuinasa saini yake.

Simba imeingilia  kati baada ya kumalizana na Kiungo wao Clatous Chama ambaye naye ametambulishwa Yanga, huku kukiwa na taarifa za kwamba Chama bado anahitaji kusalia Simba na alimalizana na Mohammed Dewji.

Ugumu wa Simba kumsajili Fei Toto ni pale ambapo Yanga wanatakiwa kujulishwa kwanza, biashara yeyote kumhusu mchezaji huyo.

Hichi kipengele cha kwenye mktaba wa makubaliano kati ya Azam FC na Yanga SC walikiweka,  ili Vilabu hivyo viwili viendelee kunufaika na mchezaji huyo popote anapoenda.

JE SIMBA IFANYEJE KUMSAJILI FEI TOTO?

Kwenye mauzo ya Fei Toto kwenda Azam,klabu ya Yanga iliweka kipengele cha kulipwa Tsh bilion moja endepo Azam FC watamuuza Feisal moja kwa moja kwenda Simba.

Njia pekee ya Azam kukwepa kipengele hicho ni kumuuza Fei Toto kwenye klabu Nyingine Hapa nchini Kisha atatokea huko kwenda Simba SC.

Mfano Azam FC wanaweza kumuuza Fei Toto kwenye klabu ya Mtibwa au Coastal,Kisha atatoka huko na kujiunga na Simba moja kwa moja.

SOMA NA HII  NABI AMPA WOSIA HUU AZIZ KI...AMCHANA MAKAVU LIVE...AMEZUNGUMZA HAYA