Home Habari za michezo TAIFA STARS YAPANDA VIWANGO VYA CAF YAIPIKU TUNISIA

TAIFA STARS YAPANDA VIWANGO VYA CAF YAIPIKU TUNISIA

0

Tanzania imepanda kwa nafasi moja katika chati ya viwango vya ubora vya nchi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), kulingana na mafanikio ya klabu kwenye mashindano ya Afrika.

Chati hiyo inatokana na tathmini ya ushiriki wa miaka mitano wa klabu za nchi husika katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika.

Tanzania ambayo ilikuwa nafasi ya sita, sasa ipo nafasi ya tano huku Tunisia iliyokuwa nafasi ya tano ikishuka hadi ya sita.