Kwa upande wa Barberian FC zamani Kiluvya United, msimu huu umekuwa ni mgumu zaidi kwa timu hiyo na inashika nafasi ya 16, ikiburuza mkiani na pointi 10, baada ya kushinda mechi moja tu, sare saba na kupoteza 14 kati ya 22.
Uhondo wa ligi hiyo utaendelea tena kesho Jumapili kwa mechi tatu kupigwa na Mbuni FC iliyochapwa na Gunners FC ya Dodoma mabao 3-2, itakuwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri, Abeid, jijini, Arusha kuikaribisha Stand United ‘Chama la Wana’.
Mbuni FC inayoshika nafasi ya sita na pointi 38, imeshinda mechi 12, sare mbili na kupoteza nane, huku kwa upande wa Stand United yenye kumbukumbu ya kuchapwa na TMA FC mabao 4-2, ikiwa nafasi ya 13, baada ya kukusanya pointi zake 20.
Kwenye Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Chunya, jijini, Mbeya, KenGold iliyochapwa na Mbeya Kwanza mabao 4-1, mechi iliyopita, itabakia nyumbani kwa kukikaribisha Bigman FC, kilichotoka pia kuchapwa na Songea United bao 1-0.
Kwa msimu wa 2023-2024, KenGold ilitwaa ubingwa wa Championship, ikiibuka kinara na pointi 70, ikiungana na Pamba Jiji ya Mwanza iliyomaliza nafasi ya pili na pointi 67, iliyorejea Ligi Kuu, baada ya miaka 21, tangu iliposhuka mwaka 2001.
Hata hivyo, KenGold ilishindwa kumudu presha za Ligi Kuu Bara na kushuka daraja msimu wa 2024-2025, ikimaliza mkiani na pointi 16, ikishinda mechi tatu tu, sare saba na kupoteza 20, ikiungana na Kagera Sugar, iliyomaliza ya 15 na pointi 23.
Baada ya TMA FC kuichapa Stand United mabao 4-2, itakuwa uwanja wake wa nyumbani kuikaribisha Gunners FC kutoka jijini, Dodoma, yenye kumbukumbu nzuri, baada ya mechi iliyopita kushinda mabao 3-2, dhidi ya Mbuni FC ya Arusha.
Kocha wa African Sports, Ally Salimu Mdoe ‘Bai’, amesemamalengo ya timu hiyo kwa sasa ni kupambana katika mechi nane zilizobakia, ili kukitoa kikosi hicho katika nafasi za kucheza mtoano (Play-Off), licha ya ushindani pia mkubwa uliopo.