Kwa sasa, mshambuliaji huyo ameweka kipaumbele chake katika kuisaidia Atletico Madrid kutwaa taji lao la kwanza la Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kuelekeza nguvu zake kwenye Kombe la Dunia akiwa na Argentina.
Wakati huo huo, Arsenal wanapanga kufanya usajili mkubwa mwishoni mwa msimu, wakilenga kuongeza mshambuliaji, kiungo wa kati pamoja na beki wa pembeni ili kuimarisha kikosi chao.