Alifikia mabao 50 katika mechi 66, ikiwa ni haraka zaidi kuliko wengi, nyuma ya Haaland (49 mechi) na Van Nistelrooy (62 mechi). Idadi ya mechi 66 ni sawa na ile ya Messi alipofikia mabao 50.
THIERRY HENRY (MABAO 50)
Thierry Henry alifunga mabao 50 katika Ligi ya Mabingwa akiwa na klabu tatu, Arsenal (35), Barcelona (8) na Monaco (7). Alianza vizuri akiwa Monaco akifunga mabao sita katika mechi tano za kwanza akiwa na umri wa miaka 20 kabla ya kuhamia Arsenal msimu wa 1999-2000. Mabao yake 35 kwa Arsenal yanamfanya kuwa mfungaji bora wa klabu hiyo katika historia ya mashindano hayo.
MOHAMED SALAH (MABAO 50)
Mohamed Salah alifikia mabao 50 ya Ligi ya Mabingwa Ulaya katika ushindi wa Liverpool dhidi ya Galatasaray, Machi 2026.
Kwa bao hilo, alikuwa mchezaji wa kwanza kutoka Afrika kufikia alama hiyo katika historia ya mashindano hayo.