Licha ya kwamba tayari Burnley imeshashuka daraja, lakini Zeki Amdouni alirejea uwanjani baada ya kukaa nje siku 291 kutokana na majeraha ya goti. Katika msimu mbaya wa Burnley, kurejea kwake ni habari njema kwa mashabiki. Kocha wa muda, Mike Jackson, anaweza kutumia mchezo dhidi ya Aston Villa kumpa nafasi ya kuonyesha uwezo na kuwapa matumaini mashabiki waliokata tamaa mapema.
7. CRYSTAL PALACE KUAMUA BINGWA?
Licha ya Crystal Palace kutokuwa salama kabisa dhidi ya kushuka daraja, kocha Oliver Glasner anaweza kupumzisha baadhi ya nyota wake dhidi ya Everton kutokana na uchovu wa Conference League. Lakini, mchezo dhidi ya Manchester City wiki ijayo unaweza kuwa muhimu zaidi katika mbio za ubingwa. Ikiwa Palace bado watahitaji pointi kujinusuru, wanaweza kucheza kwa nguvu zote dhidi ya City. Baadaye watakutana na Brentford na Arsenal, hivyo wanaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuamua bingwa wa Ligi Kuu.
8. ELANGA KUREJEA NYUMBANI
Anthony Elanga anatarajiwa kurejea sehemu anayojulikana zaidi Nottingham Forest kabla hajatimkia alipo sana. kocha wake, Eddie Howe anataraji kubakia Newcastle United baada ya msimu kumalizika, hivyo anatumia mechi zilizobaki kuamua nani ataendelea naye. Elanga, Nick Woltemade na Anthony Gordon walibaki benchi katika ushindi dhidi ya Brighton.
Lakini, Elanga kwa sasa anarudi City Ground ambako aliwahi kung’ara akiwa Nottingham Forest. Mazingira anayoyafahamu yanaweza kumsaidia kuonyesha ubora wake tena dhidi ya timu inayomjua vizuri.
9. PABLO FELIPE VS ARSENAL
Supastaa wa West Ham United, Pablo Felipe anatakiwa kuonyesha uwezo mkubwa dhidi ya Arsenal katika mechi yenye uamuzi kuhusu hatima ya timu zote mbili.
Felipe amekuwa akijituma tangu ajiunge na West Ham kutoka Gil Vicente, Januari, mwaka huu, lakini bado hajafunga bao. West Ham walimnunua kwa Pauni 18.3 milioni na bado wanaamini ana uwezo mkubwa. Tatizo ni kwamba hajatoa mchango mkubwa wa mabao. Katika mechi 11 za ligi ana asisti moja tu. West Ham sasa wako kwenye hatari ya kushuka daraja na wanahitaji straika huyo aanze kufunga, ingawa kufanya hivyo dhidi ya Arsenal sio kazi rahisi.
10. MADDISON KURUDI NA JAMBO SPURS?
Tottenham Hotspur wana presha kubwa katika vita vya kushuka daraja, lakini ushindi wa hivi karibuni umeongeza matumaini ya kusalia Ligi Kuu England.
Kurudi kwa kiungo wao, James Maddison, kwenye kikosi kumeonekana kuleta hamasa kubwa, licha ya kuwa hajaingia uwanjani tangu apone jeraha kubwa la goti. Kocha Roberto De Zerbi amesema uzoefu na utulivu wa Maddison ni muhimu kwa timu na ikiwa ataingia hata kwa dakika chache dhidi ya Aston Villa inaweza kuwa nguvu mpya kwa Spurs katika mwisho huu mgumu wa msimu kwao.