Yanga SC
OKELLO AWEKA WAZI MSIMAMO WAKE KULINGANISHWA NA CHAMA
Vardo
May 24, 2026
8:28 pm
KIUNGO mshambuliaji wa Allan Okello amefunguka kuhusu mjadala unaoendelea miongoni mwa mashabiki wa soka wa Tanzania wa kumlinganisha na nyota wa Clatous Chama, akisisitiza kuwa hana tatizo na mjadala huo bali unamchochea kuongeza bidii uwanjani.
Okello amesema anamuona Chama kama mchezaji mwenye ubora mkubwa ambaye amekuwa akimfuatilia kwa muda mrefu, hata kabla hajajiunga rasmi na Yanga SC, jambo linaloonyesha heshima aliyonayo kwa kiungo huyo wa mpinzani wake wa jadi.
Kauli hiyo imeendelea kuamsha mjadala mkali mitandaoni na vijiweni, mashabiki wa soka wakigawanyika kuhusu nani bora zaidi kati ya wawili hao wanaoonekana kuwa injini muhimu katika timu zao.
Tangu kurejea kwake Simba SC Januari 2026, Chama ameendelea kuwa na mchango mkubwa akiwa na mabao manane na asisti sita, takwimu zinazomuweka katika kiwango bora zaidi pamoja na kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mechi mara tano mfululizo mwezi Mei.
Kwa upande mwingine, Okello naye ameonyesha makali yake ndani ya Yanga SC tangu Januari 2026, akifunga mabao tisa na kuwa miongoni mwa wachezaji wenye mchango mkubwa wa mabao kikosini, akizidi hata baadhi ya washambuliaji waliopo kwenye kikosi hicho.
Okello amesisitiza kuwa hashawishwi na mjadala wa nani bora kuliko mwingine, akisema anautumia kama motisha ya kuongeza juhudi zaidi uwanjani na kusaidia Yanga SC kufikia malengo yao ya msimu.