Chipukizi FC Yafanya Kufuru: Yashusha Mashine 6 Mpya na Kocha Mpya Ligi Kuu Zanzibar 2026/2027
Zikisalia takribani siku 20 kabla ya kuwashwa kwa moto wa Ligi Kuu Zanzibar msimu wa 2026-2027, klabu ya Chipukizi FC imeendelea kuonyesha nia ya dhati ya kupambania ubingwa msimu huu baada ya kufanya maboresho makubwa kwenye benchi la ufundi na kikosi chake.
Kocha Mpya Kusuka Mipango
Maboresho hayo yalianza rasmi kwa kumtambulisha kocha mzoefu, Suleiman Mohammed ‘Mani Gamera’, aliyekuwa akiifundisha timu ya Fufuni msimu uliopita. Mani Gamera anachukua mikoba hiyo akiwa na jukumu la kuijenga Chipukizi yenye ushindani wa kweli.
Wachezaji 6 Wapya Watambulishwa
Ili kuimarisha kikosi hicho, Chipukizi imekamilisha usajili wa nyota sita wapya tayari kwa vita ya msimu mpya:
-
Dady Hiluka – Aliyekuwa mchezaji wa Mtibwa Sugar iliyoshiriki Ligi Kuu Bara msimu wa 2025-2026.
-
Kimu Juma
-
Salum Kifigo
-
Suleiman Kibadeni
-
Haruni Ndile
-
Canille Mgonela
Akizungumza kuhusu usajili huo, Kocha Mani Gamera amebainisha kuwa wachezaji hao ndio nguzo kuu inayotazamiwa kuleta mabadiliko makubwa uwanjani. Tayari kikosi hicho kimeshaanza mazoezi makali ili kujiweka sawa kabla ya ligi kuanza.
“Chipukizi ya msimu huu itakuwa tofauti kabisa na misimu iliyopita. Tumejipanga kushindana na kupigania nafasi za juu na si kucheza kwa hofu ya kushuka daraja kama ilivyozoeleka,” alisisitiza Kocha Mani Gamera.
Walioonyeshwa Mlango wa Kutokea (Kutemwa)
Katika hatua nyingine ya kupunguza mzigo na kupisha damu changa, klabu hiyo imeachana na wachezaji 12. Orodha ya walioachwa inajumuisha:
-
Mashir Khamis Sabur
-
Mahir Khamis Sabur
-
Ayoub Moh’d Abdallah
-
Job Song
-
Bille Mwakysa
-
Sadat Abdallah
-
Omar Kanyoro
-
Ali Moh’d Ali
-
Morata
-
Abdulraut Haji Makame
-
Said Suleiman Matar
-
Shaban Ali Geda