Uncategorized

TANZIA: MJUMBE KAMATI YA UTENDAJI YANGA AFARIKI

admin May 31, 2019 8:34 am

TIMU ya Yanga pamoja na familia ya wanamichezo duniani imepata pigo kufuatia kifo cha mjumbe wa kamati ya Yanga Felix Kibodya.

Kibodya amefariki usiku wa kuamkia leo Ijumaa hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda.

Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela amethibitisha taarifa hizo za kifo cha Kibodya.
Mwakalebela amesema Yanga imepata pigo kutokana na msiba huo kwani walikuwa wanategemea nguvu kubwa kutoka kwa marehemu juu ya taaluma yake ya sheria.

Mwakalebela ameongeza kuwa kwa sasa klabu yao inafuatilia msiba huo kwa karibu kujua utaratibu kamili na kwamba baada ya hapo watatoa taarifa.

HAWA HAPA WALIOTWAA TUZO ZA MO Yanga walivaa ovyo kwenye futari, Simba walifundisha kuvaa Yanga Jana.

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply