Uncategorized

LACAZETTE AIBUA MASWALI KUPITA MITAA YA BARCELONA

admin June 3, 2019 8:39 am

STRAIKA wa Arsenal, Alexandre Lacazette ameonekana katika mitaa ya jiji la Barcelona juzi na kuzua maneno.

 Baada ya kuonekana huko, ndio wadau wa soka wakadai kuwa Lacazette huenda ametua kukutana na viongozi wa klabu ya soka.
Barcelona inajulikana inasaka straika wa kati na miongoni mwa mastaa akiwemo Lacazette . Lacazette amepachika mabao 19 katika mechi 48 ambazo ameichezea Arsenal msimu wa 2018/19.
Klabu hiyo inatafuta mbadala wa Luiz Suarez, ambaye umri unazidi kumtupa mkono akiwa na umri wa miaka 32. Ili kumpata straika huyo basi Barcelona itapaswa kupanga bajeti ya kiasi cha pauni milioni 57.
Hata hivyo, taarifa zinasema kuwa fowadi huyo yupo kwa mapumziko katika mji wa Barcelona baada ya kumalizika kwa msimu.
MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMATATU SAMATTA AWASHUKURU WATANZANIA KWA SAPOTI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply