Uncategorized

BAADA YA SIKU 23, OKWI KUKINUKISHA SIMBA

admin June 26, 2019 6:44 am


HUKO ulipo weka kumbukumbu kabisa kwamba itakapofika Julai 19, straika wa Simba, Emmanuel Okwi ndiyo itakuwa siku ambayo ataanika juu ya mustakabali wake ndani ya kikosi hicho.

Okwi amemaliza mkataba wake ndani ya Simba ambapo kwa sasa straika huyo amekuwa akichengachenga kusaini mkataba mpya ndani ya kikosi hicho.

Mshambuliaji huyo ambaye kwa sasa yupo na timu ya taifa ya Uganda kwenye michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (Afcon), ameweka wazi kwamba itakapofika Julai 19, siku ambayo michuano hiyo inayofanyika nchini Misri kufikia tamati, ndipo atatoa msimamo wake wa kubakia ama kuondoka Simba.

Kuanzia leo hadi Julai 19, mwaka huu, zitakuwa zimepita siku 23 ambapo ndipo Okwi ataweka wazi mustakabali wake. “Hilo swali la mimi kubakia au kuondoka hapa Simba jibu lake litapatikana baada ya kumalizika kwa mashindano haya ya Afcon,” alisema Okwi.

Okwi anatarajiwa kuondoka Simba baada ya awali kuelezwa kuwa anataka kwenda Afrika Kusini au nchini Misri. Hata hivyo, Simba bado wanaonekana kuwa wanataka saini ya mshambuliaji huyo mahiri kwenye soka la Tanzania.

BALINYA AMTIKISA KAGERE BONGO MRITHI WA NDAYIRAGIJE NDANI YA KMC HUYU HAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply