Uncategorized

Mimi ni shabiki wa Mtibwa na siyo Simba-Juma Kaseja

admin June 27, 2019 9:53 am

Wakati watu wengi wakiamini Juma Kaseja ni shabiki wa Simba Sc kutokana na yeye kucheza kwa muda mrefu katika klabu hiyo ya Kariakoo, leo amedhibitisha rasmi kuwa yeye siyo shabiki wa Simba.

“Mimi siyo shabiki wa Simba SC, wakati mimi naanza kudaka timu ambayo ilikuwa juu ni Mtibwa Sugar. Ndiyo timu ambayo nilianza kuipenda”.

“Kuna watu hawajui , mimi nimeshawahi kudaka Mtibwa Sugar kwenye mechi moja dhidi ya Yanga. Miaka ya 2000 ndiyo miaka ambayo Mtibwa Sugar ikibeba ubingwa mara mbili mfululizo”. Alidai golikipa huyo wakati anazungumza na kituo cha radio cha East Afrika Radio.

“Mtibwa ndiyo sehemu ambayo nilitamani kucheza kwenye maisha yangu ya soka yote. Natamani kwenda kumalizia maisha yangu ya mpira kwenye klabu hiyo ya Mtibwa Sugar “- alimalizia golikipa huyo wa zamani wa Yanga na Simba.

The post Mimi ni shabiki wa Mtibwa na siyo Simba-Juma Kaseja appeared first on Kandanda.

HILI NDILO BALAA LA MBRAZIL MPYAA ALIYETUA SIMBA, SI WA MCHEZO MCHEZO EXCLUSIVE: KAPOMBE AONGEZA MIAKA MIWILI MIWILI SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply