Uncategorized

SONSO AJA NA MKWARA YANGA

admin July 1, 2019 9:20 am


BEKI mpya wa Yanga, Ally Mtoni Sonso amesema kuwa alikuwa na ndoto kubwa sana ya kucheza na Yondani na baada ya kusajiliwa na Yanga amesema wapinzani wakae pembeni.

Sonso juzi Ijumaa akiwa nchini Misri na timu ya Taifa ya Tanzania alisajiliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili akitokea timu ya Lipuli FC ya mkoani Iringa.

Sonso ameliambia Spoti Xtra kuwa, alikuwa na ndoto ya kucheza na Yondani kwani ni beki bora kwake na anaamini kuwa kama wakicheza pamoja hakuna mshambuliaji yeyote wa kumsumbua.

“Yondani ni beki mzuri sana hakuna asiyefahamu hilo na mimi nilikuwa natamani siku moja nicheze naye timu moja kwani kwa uwezo wake mzuri alionao tukicheza wote hakuna mtu wa kutusumbua kabisa,’’ alisema beki huyo.

WENGINE SIMBA KUTIMKIA AFRIKA KUSINI SIMBA YAINGIA MKATABA NA KAMPUNI YA A-ONE, YAVUNA MAMILIONI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply