Uncategorized

KOCHA MPYA YANGA AANZA KAZI NA KINDOKI

admin July 14, 2019 2:35 pm


KOCHA wa makipa ndani ya Yanga, Peter Manyika amesema kuwa ameanza kazi na mlinda mlango Klaus Kindoki ambaye msimu uliopita mashabiki hawakumkubali kutokana na kufanya makosa mengi ya kiufundi.

Moja ya mechi ambayo Kindoki alifanya makosa ya kiufundi ni kwenye mchezo wake wa kwanza dhidi ya Stand United ambapo aliruhusu kufungwa mabao 3 na Alex Kitenge licha ya Yanga kushinda kwa mabao 4-3.

Akizungumza na Saleh Jembe, Manyika amesema kuwa ameangalia namna bora itakayomfanya awe katika ubora wake msimu ujao.

“Nimeanza na kuangalia namna bora ya kumrejesha kwenye ubora wake mlinda mlango Kindoki, msimu uliopita alifanya makosa mengi ya kiufundi hicho ndicho tunachokifanyia kazi, nina imani kwa programu ambayo wataifanya mambo yatakuwa safi,” amesema.

Manyika amechukua nafasi ya Juma Pondamali ambaye amesema kuwa kwa sasa anataka kufanya kazi nyingine mbali na mpira.

JOSE MOURINHO ASAKA TIMU YA KUFUNDISHA ADAI ANA HASIRA NA KAZI KAGERE AKIMBILIA GYM

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply