Uncategorized

MBAO WAPO VIZURI, KUANZA KAZI NA AALIANCE FC

admin August 20, 2019 9:59 am


UONGOZI wa Mbao FC umesema kuwa umekamilisha mipango kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuanza Agosti 24.

Mbao FC kwa sasa ipo chini ya Kocha Mkuu, Hemed Morroco baada ya kuachana na Salum Mayanga ambaye ametua Ruvu Shooting.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mwenyekiti wa Mbao FC, Solly Njashi amesema wamejipanga kiasi cha kutosha kuleta ushindani. 


“Kikosi kipo salama na kinaendelea kukamilisha maandalizi ya mwisho, tunajua kwamba mashabiki wanahitaji burudani nasi tunachofanya ni kuandaa mipango makini.

 “Muda wetu wa kufanya vema ni sasa kwani tunaanza na ndugu zetu Alliance lazima tufanye kweli,” amesema.

Mchezo wa Kwanza kwa Mbao utakuwa dhidi ya Alliance utachezwa Uwanja wa Kirumba Agosti 24 na Alliance atakuwa mgeni.

JEZI YA EMANUEL OKWI NI 19 SIO 7 TENA MBEYA CITY WAO WAIKOMALIA TANZANIA PRISONS

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply