Uncategorized

AZAM FC YAPANIA KUFANYA MAKUBWA MBELE YA WAZIMBABWE

admin September 5, 2019 11:28 am


UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa upo tayari kupeperusha bendera ya Taifa Kimataifa kwa kupata matokeo chanya mbele ya Triangle FC ya Zimbabwe.

Mchezo huo ambao unatarajiwa kuchezwa kati ya Septemba 13-15 uwanja wa Chamazi ni wa hatua ya kwanza ya Kombe la Shirikisho utapingwa majira ya saa 10:00 jioni.

Idd Cheche, Kocha Msaidizi wa Azam FC amesema kuwa maandalizi yanakwenda sawa na kikosi kipo vizuri kupeperusha bendera ya Taifa.

“Tunatambua kwamba utakuwa mchezo mgumu na kila mchezaji anahitaji kupata matokeo ni suala la muda na mashabiki watupe sapoti kwa kuwa tunaanza nyumbani kisha tunakwenda kumaliza tukiwa ugenini,” amesema. 

YANGA YAZIPIGIA HESABU NDEFU PESA ZA CAF BEI MPYA ZA VING’AMUZI VYA DSTV, MAMBO KWA ULAINII….

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply