Uncategorized

YANGA YATUMA UJUMBE HUU KWA MASHABIKI, KAZI YAO NI MOJA TU KIMATAIFA

admin September 5, 2019 2:38 pm


UONGOZI wa Yanga umewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi Septemba14 ili kuwapa sapoti wachezaji wakipambana kwenye mchezo wa hatua ya kwanza na wa kimataifa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mratibu wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kuwa kwa sasa kikosi kipo vema na kinaendelea na maandalizi kwa ajili ya mchezo huo wa kimataifa.

“Kwa sasa tupo Mwanza na tunaendelea kujipanga kwa ajili ya mchezo wetu wa kimataifa dhidi ya Zesco, tunatambua kwamba haitakuwa kazi nyepesi ila tupo tayari.

“Mashabiki wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti na kuwashangilia wachezaji ni jambo la busara na muhimu kwani timu ni yetu sote na lengo letu ni kufanya vizuri,” amesema.

NYOTA MWINGINE WA SIMBA ATIMKIA KUKIPIGA ASIA KOCHA SIMBA ATOA ELIMU YANGA NAMA YA KUWAMALIZA ZESCO, AMTAJA YONDANI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply