Uncategorized

KAZI NDO KWANZA IMEANZA, CHIRWA AWA MTAMU KABLA YA KUWAVAA WAZIMBABWE

admin September 8, 2019 11:03 am


OBREY Chirwaa ameanza kuwa mtamu ndani ya Azam FC baada ya jana kufanya maajabu yake kwa kufunga ‘hattrick’ kwenye mchezo wa kirafiki.

Azam FC ambayo inajiaanda na mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Triangel United ya Zimbabwe Septemba 15 kwa sasa imecheza jumla ya michezo mitatu ya kirafiki.

Kwenye michezo miwili ambayo walicheza dhidi ya Transit Camp ambapo walishinda mabao 3-1, Friends Rangers ambao walishinda mabao 3-0, Chirwa hakufunga hata bao moja na ameibuka jana kwa kufunga mabao matatu wakati wakiibuka na ushindi wa mabao 4-1 mbele ya Pan Africans mchezo uliochezwa uwanja wa Chamazi.

Safu ya ulinzi ya Azam FC inayosimamiwa na Nicholaus Wadada imeruhusu jumla ya mabao mawili huku safu ya ushambuliaji ikifunga jumla ya mabao 10.

Idd Cheche , Kocha Msaidizi wa Azam FC amesema kuwa ni mwendelezo wa kufuta makosa ya safu ya ushambuliaji ambayo yamekuwa pasua kichwa ndani ya kikosi.

MASHABIKI MIA TANO KIMEELEWEKA LEO TAIFA, AZAM SIO WA MCHEZOMCHEZO KIKOSI CHA STARS DHIDI YA BURUNDI HIKI HAPA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply