Uncategorized

KLOPP ANA MATUMAINI YA KUTOSHA KWA MANE, MJAPAN AKICHAFUA KWA MARA YA KWANZA

admin January 24, 2020 5:26 am

JURGEN Klopp, Kocha Mkuu wa Liverpool ana matumaini kwamba majeruhi aliyopata mshambuliaji wake Sadio Mane sio makubwa sana atarejea Uwanjani hivi karibuni.

Mane aliumia kwenye mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Wolves, Jana, Januari 23, kipindi cha kwanza baada ya kucheza dakika 30 na nafasi yake ilichukuliwa na Takumi Minamino, mshambuliaji mpya wa Liverpool aliyekuwa benchi.

Mchezo dhidi ya Woves unakuwa ni wa kwanza kwa Mjapan Minamino kucheza ndani ya Ligi Kuu England baada ya kumwaga kandarasi ndani ya timu hiyo akitokea Red Bull Salzburg.

Liverpool ilishinda kwa jumla ya mabao 2-1 kwenye mchezo huo ambapo mabao ya Liverpool yalifungwa na Jordan Henderson kwa kichwa dakika ya nane na lilisawazishwa dakika ya 51 na Wolves kupitia kwa Raul Jimenez dakika ya 51 na lile la ushindi likipachikwa na Roberto Firmino kwa Liverpool dakika ya 84.

Ushindi huo unaifanya Liverpool kufikisha jumla ya pointi 64 ikiwa kileleni, ikiwaaacha kwa tofauti ya pointi 16 mabingwa watetezi Manchester City wenye pointi 51 huku Wolves ikiwa nafasi ya 7 na pointi zake 34.
AZAM FC SASA WAMEHAMIA HUKU, KUANZA LEO KAZI AZAM TV YAZINDUA APP MPYA YA AZAM TV MAX

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply