Uncategorized

NAMUNGO FC YAZIPIGIA HESABU POINTI TATU ZA MWADUI FC

admin February 14, 2020 2:07 pm


HITIMANA Thiery, Kocha Mkuu wa Namungo FC amesema kuwa kikosi chake kipo sawa na kinaendelea na maadalizi kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mwadui FC utakaopigwa Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Namungo FC imetoka kuichapa bao 1-0 Singida United imefikisha jumla ya pointi 36 baada ya kucheza mechi 20 ipo nafasi ya nne.

Thiery amesema kuwa :”Kila mechi ni ngumu na wanachotazama ni kupata matokeo mazuri kutokana na ugumu ambao wanakutana nao na anaamini watafanya vizuri.

“Kila mechi kwetu ni muhimu kupata ushindi na kilichobaki kwa sasa ni kuona namna gani ambavyo tunaweza kupata pointi tatu muhimu,”.

LIPULI:NJOONI SAMORA MPATE BURUDANI MZUNGU WA YANGA:HUYO MOLINGA MTAMUELEWA TU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply