Uncategorized

SABABU ZA MAKOCHA MBAO FC KUBWAGA MANYANGA HII HAPA

admin February 18, 2020 11:22 am


HEMED Morocco na msaidizi wake Abdulmutik Hajji wameachana na timu ya Mbao FC ya mkoani Mwanza.

Morocco amesema kuwa sababu kubwa ya kuachana na tim hiyo ni matokeo mabovu ambayo wamekuwa wakiyapata.

Mbao FC ina pointi 19 ipo nafasi ya 18 imecheza mechi 22, imeshinda michezo minne, sare saba na imepoteza michezo 11.

Mwenyekiti wa Mbao FC, Solly Njash amesema kuwa kwa sasa wapo kwenye mchakato wa kumtafuta kocha mpya atakayenoa kikosi hicho.


“Tunatoa shukran kwa kazi nzuri na ushirikiano waliotupa kipindi chote tulipokuwa nao na tunawatakia kila la kheri, kwa sasa tunafanya mchakato wa kumtafuta kocha mpya,” amesema.

SIMBA YAOMBA SAPOTI KUTOKA KWA MASHABIKI JESHI LA YANGA LITAKALOANZA LEO DHIDI YA POLISI TANZANIA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply