Uncategorized

KILE KICHAPO CHA BAO 1-0 WALICHOPOKEA SIMBA KUTOKA KWA YANGA CHAIBUA HAYA

admin March 10, 2020 9:27 pm


CLATOUS Chama, kiungo mshambuliaji wa Simba amesema kuwa ameumia kwa timu yake kuchapwa bao 1-0 mbele ya Yanga kwenye mchezo wao uliochezwa Machi 8 Uwanja wa Taifa jambo linalomfanya apoteze furaha kama ilivyo kwa mashabiki wa Simba.

Kichapo cha Simba ilichokipata mbele ya Yanga kimewafanya wapinzani wao wafikishe pointi 50 kwenye ligi na mabao 30 huku Simba ikibakiwa na pointi zake 68 na mabao 55.

Chama amesema: “Nimeumia na matokeo mabaya ambayo tumeyapata, sikutarajia kuona haya yanatokea ila mwisho wa siku ni mchezo na tumeyapokea matokeo tunajipanga kwa ajili ya mechi zetu nyingine,” .

Chama ni kinara wa pasi za mwisho ndani ya Simba akiwa ametoa pasi saba na amefunga mabao mawili.

YANGA KWENYE KIBARUA KINGINE KESHO TAIFA MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMATANO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply