Uncategorized

KIWANGO CHA LUIS CHAMFANYA MUSA MGOSI KUSEMA HAYA..!!

admin April 11, 2020 12:08 pm

NAHODHA wa zamani wa Simba ambaye ni miongoni mwa wachezaji waliojenga heshima Msimbazi, Musa Hassan ‘Mgosi’ amesema winga Luis Miquissone anaitendea haki jezi yake.

Katika mahojiano maalumu na Mwanaspoti, Mgosi ambaye alikuwa anavaa jezi namba 11 ambayo anaitumia mchezaji huyo raia wa Msumbiji amesema tangu atundike daruga mwaka 2016 hakuna mchezaji aliyeitumia vyema namba hiyo kama anavyofanya Luis.

Anasema jambo hilo pekee limefanya ajione amerejea upya uwanjani kutokana na kiwango cha nyota ambaye amefunga magoli matatu hadi sasa tangu asajiliwe wakati wa dirisha dogo la usajili msimu huu. Awali tangu Mgosi aondoke jezi hiyo imewahi kuvaliwa na Laudit Mavugo, Marcel Kaheza na Wilker da Silva.

Luis ameonekana kuwapa raha mashabiki wa timu hiyo, huku wakitarajia kuona makubwa zaidi kwake kama alivyoahidi bado hajafikia kiwango anachokitaka.

“Hakuna mchezaji duniani kote ambaye akistaafu atafurahia jezi yake ikivaliwa na mtu mwenye kiwango duni, wakati yeye alikuwa kwenye uwezo mkubwa.

“Ndio maana nasema wachezaji wa zamani waulize watakwambia maana kuna wakati wachezaji wakicheza kiwango cha chini, wanatamani waingie wawaonyeshe ufundi ila nyakati zinakuwa zimewatupa mkono, akili zinataka miili haipo tayari,” anasema Mgosi ambaye kwa sasa ni kocha wa Simba Queens inayoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake.

YANGA YAUKATIA TAMAA UBINGWA WA LIGI KUU BARA MAZIMA ERASTO NYONI NA BAO LAKE TAIFA LILIIBUKA BAADA YA SIKU 676

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply