Uncategorized

MAN UNITED YAJIPA MATUMAINI KWA SANCHO

admin April 20, 2020 12:00 pm

London, England. Manchester United imejipa matumaini ya kushinda vita ya kuwania saini ya Jadon Sancho.

Sancho ameteka vyombo vya habari Ulaya baada ya kuzivutia  idadi kubwa ya klab zinazotaka kumwa katika usajili wa majira ya kiangazi msimu ujao.

Man United ina matumaini kumpata Sancho baada ya kuteta na klabu yake ya Borussiaa Dortmund na mchezaji husika.

Klabu hiyo italazimika kufanya kazi ya ziada kupata saini yake kwa kuwa Dortmund imepanga kumuongeza dau la mshahara ili kumbakiza.

Thamani ya Sancho inadaiwa kufikia Pauni100 milioni katika usajili wa majira ya kiangazi msimu ujao.

Sancho amekuwa katika kiwango bora tangu alipotua katika Ligi Kuu Ujerumani akifunga mabao 17 na kutengeneza mengine 19 msimu huu.

TAHADHARI NI MUHIMU, ISHU YA USAJILI ISICHUKULIWE KWA PUPA KUHUSU YANGA….CHAMA AMTAJA NIYONZIMA..!!

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply