Uncategorized

YANGA WACHEKELEA SAPOTI YA MDHAMINI KUMWAGA MKWANJA

admin April 21, 2020 6:59 am

JUMA Abdul nahodha msaidizi wa Yanga amesema kuwa mdhamini wao GSM amewaongezea nguvu ya kufanya mazoezi wakiwa nyumbani kutokana na kupewa fursa ya kufanya manunuzi kwenye duka la michezo lililopo Mlimani City.

Abdul amesema kuwa vifaa hivyo walivyonunua vitawasaidia kufanya mazoezi nyumbani kwa umakini huku wakichukua tahadhari ya Virusi vya Corona.

“Fursa ya kufanya manunuzi kwenye duka la mdhamini wetu wetu tumeifurahia na imetufanya tuwe na furaha zaidi kwani itatufanya tuendelee kufanya mazoezi nyumbani na kuendelea kuchukua tahadhari ya Virusi vya Corona,” amesema.

HIKI NDICHO ANACHOKIFANYA FEI TOTO MANCHESTER UNITED, BARCELONA ZAKUTANA KWA MTUPIAJI HUYU FUNDI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply