Uncategorized

LUSAJO BANA, APATA KIGUGUMIZI KUZUNGUMZIA DILI LAKE LA YANGA

admin May 5, 2020 3:57 pm


RELLIANTS Lusajo, mshambuliaji namba moja wa Klabu ya Namungo FC amesema kuwa hawezi kuzungumzia juu ya dili lake la kutua ndani ya Klabu ya Simba ama Yanga kwa sasa kwa kuwa bado ana mkataba kwenye klabu yake.

Lusajo inaelezwa kuwa yupo kwenye hesabu za mabosi wake wa zamani Yanga ambao wanahitaji saini yake huku Simba pia wakiiwinda saini yake.

Akizungumza na Saleh Jembe, Lusajo amesema:”Nina mkataba na Namungo kwa sasa siwezi kuzungumza kuhusu ishu ya kwenda Yanga ama Simba.

“Ni kweli mkataba wangu upo karibu kuisha ila haina maana kwamba ndio nishajua kuwa wapi nitasaini hapana, nangoja mkataba uishe kwanza,” amesema Lusajo.

Lusajo ametupia mabao 11 ndani ya Namungo FC inayofundishwa na Hitimana Thiery.

YANGA WAMTAJA MCHEZAJI WA SIMBA KUWA NDIYE BORA NDANI YA LIGI KUU BARA MTIBWA WAKAZA, WAGOMA KURUDI KAMBINI KWA SASA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply