Uncategorized

JUMA KASEJA:WACHEZAJI WENGI VIWANGO VITAPOROMOKA

admin May 16, 2020 11:28 am

JUMA Kaseja kipa mkongwe ndani ya ardhi ya Bongo anayekipiga ndani ya Klabu ya KMC amesema kuwa wachezaji wengi wameshuka viwango kutokana na kukaa muda mrefu bila kucheza. 

Machi 17,2020 Serikali ilizuia mikusanyiko isiyo ya lazima pamoja na ligi zote kusimamishwa kutokana na mlipuko wa Virusi vya Corona ambavyo vinaivurugavuruga dunia.

Kaseja amesema:”Mchezaji yeyote atakayekaa nje ya Uwanja zaidi ya mwezi mmoja bila kucheza na kufanya mazoezi ya nguvu lazima kiwango chake  kitaporomoka hivyo wachezaji wengi wamekumbwa na hali hiyo kwa kuwa wamekaza muda mrefu bila kucheza.

 “Wachezaji wengi wamekosa mazoezi na mechi nyingi naona kutakuwa na ngumu sana kama Ligi ikirejea tena kwani kutakuwa na kazi ya ziada kwa wachezaji kurejesha viwango vyao.”

CLATOUS CHAMA WA SIMBA AWATAJA WAARABU TAIRONE YULE BEKI MBRAZILI WA SIMBA AMETOA YA MOYONI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply