Uncategorized

WINGA AS VITA AKUBALI KUTUA YANGA

admin May 17, 2020 9:58 pm

WINGA machachari wa AS Vita, Tuisila Kisinda, amesema kuwa Yanga ndiyo timu ambayo ipo akilini mwake baada ya kufanikiwa kufanya mazungumzo ya awali na uongozi wa timu hiyo.
Yanga SC katika kuhakikisha inakijenga kikosi chao kuwa imara, imeahidi kuleta majembe kutoka timu zinazofanya vizuri katika michuano ya kimataifa kama AS Vita na timu nyingine.
Kisinda amesema kuwa kuna mazungumzo ambayo alifanya na kiongozi mmoja wa Yanga ambayo yanamfanya azidi kuifi kiria zaidi timu hiyo ambayo imeonyesha nia ya kumhitaji winga huyo.
“Nilifanya mazungumzo na mmoja wa viongozi wa Yanga, japo hatukukamilisha mipango yote ya usajili, hivyo maongezi hayo yananifanya nizidi kuifikiria Yanga kwa kuwa wana mpango na mimi wa kunisajili.
“Kama kila kitu kitaenda sawa huko mbeleni nadhani nitatua kwenda kucheza Yanga, kiufupi napapenda sana Tanzania kwa kuwa watu wake wanapenda amani na watulivu sana, navutiwa zaidi kucheza kwao kama nitafanikiwa,” amesema winga huyo.
AZAM FC, SIMBA WAMKUMBUKA PATRICK MAFISANGO SHEVA AANZA KUREJEA KWENYE UBORA WAKE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply