Uncategorized

YIKPE MSHAMBULIAJI WA YANGA AOMBA APEWE MUDA KUONYESHA MAAJABU

admin May 12, 2020 5:04 am
YKIPE Gislain amesema kuwa anaomba apewe

muda zaidi ndani ya Klabu ya Yanga ili kuonyesha ujuzi wake wote.

Nyota huyo alisajiliwa akitokea Klabu ya Gor Mahia ambapo alivunja mkataba wake ili kukipiga ndani ya Klabu hiyo Desemba mwaka jana.

Ameshindwa kufurukuta ndani ya Yanga ambapo amefunga bao moja ndani ya Ligi Kuu Bara ilikuwa mbele ya Singida United wakati Yanga ikishinda mabao 3-1.

Yikpe amesema:” Nataka kuondoka ndani ya Yanga nikiwa nimeweka historia na kufanya makubwa kwa ajili ya timu yangu hivyo ninahitaji nafasi. “Nimeshindwa kufanya makubwa kwa kuwa nilikuwa sipati nafasi nikipata nafasi pale ligi itakaporejea sitafanya makosa,”.

REAL MADRID HAWANA MPANGO NA RAMOS AJIBU ATAJA KILICHOMUENGUA KIKOSINI SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply