Uncategorized

NDANDA YATOSHANA NGUVU NA SIMBA NANGWANDA

admin July 5, 2020 3:47 pm


KIKOSI cha Ndanda leo kimelazimisha sare ya bila kufungana na mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Mchezo wa leo Ndanda iliyo chini ya Kocha Mkuu, Meja Mstaafu, Abdul Mingange iliingia uwanjani kwa tahadhari kubwa ikisaka ushindi ili kuweza kujinusuru kwenye hatari ya kushuka daraja.

Simba iliyo chini ya Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck haikuwa na cha kupoteza kwa kuwa tayari wameshatangazwa kuwa mabingwa.

Kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Taifa, Simba ilishinda mabao 2-0 ila leo mambo yamekuwa magumu kwa Ndanda kulipa kisasi na kufanya wagawane pointi mojamoja.

Ndanda inafikisha jumla ya pointi 37 huku Simba ikifikisha jumla ya pointi 80 kibindoni.

VPL: BIASHARA UNITED 0-0 YANGA JESHI KAZI LA AZAM FC DHIDI YA SINGIDA UNITED

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply