Uncategorized
MASHINE HIZI ZA KAZI ZIMEANDALIWA NA YANGA KUIMALIZA MTIBWA SUGAR LEO
NYOTA wawili wa Yanga, Feisal Salum, ‘Fei Totoβ na Mrisho Ngassa wameandaliwa kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara utakachoezwa leo, Julai 22, Uwanja wa Jamhuri.
Yanga ilitoka kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Mwadui FC, mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Taifa ambapo bao pekee kwa Yanga lilifungwa na kiungo, Fei Toto akimalizia pasi ya Mrisho Ngassa.
Akizungumza na Saleh Jembe, Kocha Mkuu wa Yanga, Luc Eymael amesema kuwa anafurahishwa na uwezo wa wachezaji wake jambo ambalo linampa matumaini ya kufanya vizuri kwenye mechi zake zijazo ikiwa ni dhidi ya Lipuli.
βWachezaji wangu wote wapo vizuri na bado tunapambania malengo yetu ya kumaliza ligi tukiwa nafasi ya pili hilo ili liwezekana tunahitaji kushinda mechi zetu zilizopo mbele yetu.
βKila mchezaji yupo tayari kuanzia Ngassa, Fei, Abdul (Juma) hivyo ni jambo la kusubiri kuona namna gani kazi inaweza kukamilika ndani ya uwanja, mashabiki wazidi kutupa sapoti,β amesema Eymael.
Yanga inakutana na Mtibwa Sugar iliyo nafasi ya 14 ikiwa imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 mbele ya KMC ikiwa inapambana kujinasua kushuka daraja huku Yanga ikiwa nafasi ya pili na pointi 68 zote zimecheza mechi 36.
Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.