Uncategorized

SIMBA WATIA TIMU TANGA, ALHAMISI KUVAANA NA COASTAL UNION

admin July 21, 2020 6:47 pm


KIKOSI cha Simba kimewasili salama leo Julai 21 Tanga ambapo kimekwenda kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Coastal Union unaotarajiwa kuchezwa Julai 23.

Uongozi wa Simba umesema kuwa unahitaji pointi tatu muhimu ili kuwa mwendelezo kuelekea mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Namungo FC. 

Mchezo wa fainali unatarajiwa kuchezwa Agosti 2, Uwanja wa Nelson Mandela,  Sumbawanga. 

Patrick Rweyemamu,  meneja  wa Simba amesema wana matumaini ya kupata ushindi mbele ya Coastal Union kwa kuwa wapo tayari.

“Tupo tayari kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya Coastal Union,  utakuwa mchezo mgumu kwetu lakini ni hesabu za kuelekea kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho. 

“Wachezaji wapo tayari na morali ni kubwa kwa kuwa ni kazi yao hivyo mashabiki wajitokeze kutupa sapoti kwenye mchezo wetu,” amesema. 

Simba ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 84, inakutana na Coastal Union ambayo ipo nafasi ya sita na pointi 52.

KESHO NDANI YA CHAMPIONI JUMATANO USIPANGE KUKOSA NAKALA YAKO MASHINE HIZI ZA KAZI ZIMEANDALIWA NA YANGA KUIMALIZA MTIBWA SUGAR LEO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply