Uncategorized

BREAKING:KIBWANA SHOMARI ASAINI YANGA, ATAJWA KUWA MBADALA WA JUMA ABDUL

admin August 9, 2020 12:47 pm

 

KIBWANA Shomari, beki wa kulia wa Klabu ya Mtibwa Sugar leo ametangazwa rasmi kuwa mchezaji wa Klabu ya Yanga ya Dar es Salaam,


Kibwana anaingia kwenye usajili wa Yanga na kuwa nyota wa tano kusajiliwa baada ya dirisha la usajili kufunguliwa Agosti Mosi.

Wengine waliosajiliwa Yanga ni pamoja na Bakari Mwamnyeto beki kutoka Coastal Union, Abdalah Shaibu beki wa kati, Wazir Junior mshambuliaji kutoka Mbao FC, Yasin Mustapha beki kutoka Polisi Tanzania na Zawad Mauya kiungo kutoka Kagera Sugar.

Kibwana amesaini dili la miaka miwili anatajwa kuwa mbadala wa Juma Abdul ambaye mkataba wake umeisha Yanga na hajaongezewa baada ya kushindwana na mabosi wa Yanga.
DEO KANDA ATAJWA KUIBUKIA YANGA BREAKING:SENZO AACHIA NGAZI SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply