Yanga SC

YANGA YAWATANGAZA RASMI NIZAR, NA KOCHA MGHANA

admin January 27, 2021 12:47 pm


KATIKA harakati za kuimarisha zaidi benchi lao la ufundi kuelekea mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, Klabu ya Yanga leo imewatangaza rasmi makocha wao wawili wapya ambao Nizar Khalfan na  Edem Mortotsi.

Nizar anakuja kuchukua nafasi ya kocha msaidizi iliyoachwa wazi na kocha Juma Mwambusi huku Mortotsi yeye akija kuchukua majukumu ya ukocha wa viungo pamoja na utimamu wa mwili nafasi ambayo ilikuwa wazi tangu kuondoka kwa Riedoh Berdien raia wa Afrika Kusini.

Makocha hao wawili sasa wataanza kazi rasmi chini ya Kocha Mkuu Mrundi, Cedric Kaze katika kambi ya kikosi hicho iliyoko Avic Town Kigamboni jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza baada ya utambulisho huo Mkurugenzi wa uwekezaji wa Klabu ya Yanga na Mjumbe wa Kamati ya Usajili, Injinia Hersi Said amesema: “Tuna imani kubwa na mchakato uliofanyika na kufanikisha kupatikana kwa makocha hawa wawili, kama unavyowaona wote ni vijana na wana wasifu mzuri ambao ni wazi utakuwa msaada mkubwa kwenye timu yetu katika kufikia malengo tuliyojiwekea.”

LOKOSA ATOA KAULI YA KIBABE SIMBA BREAKING: SIMBA YAMTAMBULISHA MZIMBWABE MWINGINE TENA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply