Home news UCHAGUZI RT KINAWAKA LEO

UCHAGUZI RT KINAWAKA LEO


BARAZA la Michezo Tanzania (BMT), leo linatarajiwa kusimamia uchaguzi mkuu wa Chama cha Riadha Tanzania (RT).

Uchaguzi huo ni wa kikatiba na unatarajiwa kujaza nafasi mbalimbali za uongozi katika chama hicho.

Akizungumzia kuhusu uchaguzi huo, Katibu Mkuu wa RT, Ombeni Mzavara amesema: โ€œMaandalizi yote ya uchaguzi mkuu wa chama cha riadha Tanzania yamekamilika.

โ€œKwa mwaka huu tunatarajia uchaguzi huu utasimamiwa na BMT, ambao wamehusishwa katika mchakato mzima wa uchaguzi tangu utaratibu wa kuchukua na kurudisha fomu,โ€

SOMA NA HII  YANGA vs MAMELOD NI JIWE KWA JIWE....VITA IPO KWA MASTAA HAWA....PACOME NI ZAIDI YA WOTE...