Home Taifa Stars KOCHA MKENYA AIPA MBINU STARS

KOCHA MKENYA AIPA MBINU STARS


 KOCHA mkuu wa klabu ya Biashara United, Francis Baraza amefunguka kuwa kama kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars inataka kusonga mbele katika michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN), basi ni lazima wajitahidi kutumia nafasi wanazotengeneza.

Stars kesho itacheza mchezo wake wa pili dhidi ya timu ya Taifa ya Namibia mchezo ambao Stars inahitaji kushinda ili kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele na kutinga hatua ya robo fainali, hii ni baada ya kupoteza kwenye mchezo wa kwanza mbele ya Zambia.

Baraza amekuwa na msimu mzuri kwenye ligi akiiongoza Biashara kukamatia nafasi ya nne kwenye msimamo na pointi zao 29 walizokusanya kwenye michezo 18.

Akizungumzia nafasi ya Stars Baraza amesema: “Bado naamini Stars ina nafasi ya kufuzu hatua inayofuata hii ni kama tutaweza kuwa na matumizi mazuri ya nafasi tunazotengeneza, vijana wetu wanapaswa kujituma zaidi,”

SOMA NA HII  TANZANIA YATWAA UBINGWA WA CECAFA U 23, KOCHA AWAPA TANO