Home Simba SC MORRISON AWAPA AKILI YANGA

MORRISON AWAPA AKILI YANGA


UONGOZI wa Yanga umewaondoa hofu mashabiki wa timu hiyo kwa kuwaambia kuwa mkataba wa mshambuliaji wao mpya, Fiston Abdoul Razak una kipengele cha kuongeza mwingine baada ya huo alionao kumalizika.

Hii inatokana na ukweli kwamba kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), mchezaji anapokuwa na mkataba wa miezi sita anakuwa huru kufanya mazungumzo na klabu nyingine itakayomuhitaji.

Akizungumzia mkataba huo Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Haji Mfikirwa amesema: “Niwaondoe hofu mashabiki wa Yanga kwa kuwaambia kuwa Fiston ni mali yetu na hakitatokea kitu chochote kibaya, licha ya kusaini mkataba wa miezi sita kwani yapo makubaliano mazuri kutoka pande zote mbili,”

Nyota huyo anatarajiwa kutua nchinio siku ya Ijumaa ili kukamilisha taratibu za kusaini mkataba huo.

SOMA NA HII  ALLY KAMWE: YANGA KUKOSA MAKUNDI LIGI YA MABINGWA NI UKWELI UNAOUMA...