Azam FC
AZAM FC KUMENYANA NA COASTAL UNION, LYANGA AREJEA NYUMBANI
KESHO kikosi cha Azam FC kinachonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina kitakuwa na kibarua cha kusaka pointi tatu muhimu mbele ya Coastal Union.
Msafara wa kikosi hicho chenye wachezaji 23 umewasili Tanga usiku wa jana Februari 9 ukiwa na Ayoub Lyanga mwenye jumla ya mabao matano ndani ya Ligi Kuu Bara baada ya kuwatungua Simba kwenye sare ya kufungana mabao 2-2, Uwanja wa Mkapa.
Lyanga ni zao la Coastal Union hivhivyoeo anakwenda kukutana na mabosi zake wa zamani kabla ya kesho kukutana nao ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.
Mchezo wao wa mzunguko wa Kwanza, zama za Arstica Cioaba Azam FC ilishinda mabao 2-0, Uwanja wa Azam Complex.

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.