Yanga SC

CARLINHOS ATAJA SABABU ZA KUTOKUCHEZA YANGA

admin February 16, 2021 11:47 am


KIUNGO mshambuliaji wa klabu ya Yanga, Carlos Fernandes ‘Carlinhos’ amefunguka kuwa kwa sasa tayari amekwishapona majeraha yalimweka nje ya uwanja kwa muda mrefu, na kutokuonekana kwake uwanjani kunatokana na maamuzi ya benchi la ufundi na siyo majeraha.

Carlinhos aliyejiunga na Yanga mwanzoni mwa msimu huu amekuwa akipitia kipindi kigumu cha majeraha ambayo yamemfanya kuwa nje ya uwanja tangu mwezi Novemba mwaka jana.

Nyota huyo alianza vizuri msimu huu akihusika kwenye mabao manne ya Yanga, akifunga mabao mawili na kuasisti mara mbili.

Akizungumzia maendeleo yake Carlinhos amesema: “Ni kweli hapo nyuma nilikuwa na majeraha ambayo yaliniweka nje ya uwanja kwa muda mrefu, lakini tayari nilikwishapona na kwa sasa nipo sawa kwa ajili ya kuisaidia timu yangu kupata matokeo mazuri uwanjani na kuweza kufikia malengo yetu.

“Hivyo kuhusiana na ishu ya kutokucheza, hilo ni swala lililo kwenye maamuzi ya benchi la ufundi ambayo kimsingi mimi kama mchezaji siwezi kuliongelea,”

GOMES ATAJA KITAKACHOIBEBA SIMBA KIMATAIFA FISTON ATAMBA YANGA KUMALIZA SARE MFULULIZO

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply