Simba SC

CHAMA AWAPA SIMBA BEKI WA ZAMBIA ILI WAMSAJILI

admin March 23, 2021 5:47 am


NYOTA wa Simba Clatous Chama amewaambia mabosi wake kuwa kaka yake Adrian Chama ana uwezo mkubwa uwanjani kumshinda yeye hivyo wakimpa mkataba atafurahi kucheza naye.

Chama ana miaka 29 kaka yake Chama anayecheza ZESCO United ana miaka 32 na wote wamekuwa wakipata nafasi ya kucheza timu ya Taifa ya Zambia.

Kaka yake Chama, nafasi yake uwanjani ni beki huku mdogo wake Chama anacheza nafasi ya kiungo yupo zake pia timu ya Taifa ya Zambia.

Chama amesema:”Ninajua kwamba kaka yangu ana uwezo mkubwa na anajua mpira hivyo akipata nafasi ya kucheza Simba atafanya vizuri na kuleta changamoto kwa wengine.

“Ninamjua na ninapenda kuwa naye kila mahali hivyo hakuna tatizo ikiwa Simba watamsajili watakuwa wamepata mchezaji mzuri,” .

YANGA WASIMAMISHA MAZOEZI KWA SABABU YA MAGUFULI GOMES WA SIMBA AWAPA TAHADHARI WACHEZAJI WAKE MAPEMA KIMATAIFA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply