Home Yanga SC LAMINE, MWAMNYETO WANAPATA TABU YANGA, HIVI NDIVYO WANAVYOTESEKA

LAMINE, MWAMNYETO WANAPATA TABU YANGA, HIVI NDIVYO WANAVYOTESEKA


UKUTA wa Klabu ya Yanga unaoundwa na nahodha Lamine Moro raia wa Ghana na mzawa Bakari Mwamnyeto ambaye ni msaidizi unapata tabu kwa kuokota mabao mengi nyavuni tofauti na ule wa watani zao wa jadi Simba unaoongozwa na Joash Onyango na Pascal Wawa.

Kwenye mechi tano za hivi karibuni ambazo Yanga imecheza imeruhusu jumla ya mabao 7 na kwenye harakati za kusaka pointi 15 iliambulia pointi 6 na kuyeyusha pointi 9 huku ule wa Simba ukiruhusu mabao matatu.

Mwendo wao ulikuwa namna hii:-Tanzania Prisons 1- 1 Yanga, Mbeya City 1-1 Yanga, Yanga 3-3 Kagera Sugar, Yanga 1-0 Mtibwa Sugar, Coastal Union 2-1 Yanga.

Watani zao wa jadi chini ya Wawa na Onyango kwenye mechi zao tano za hivi karibuni ndani ya ligi wameokota jumla ya mabao matatu nyavuni.

 Mbali na kuokota nyavuni mabao hayo matatu pia walipokuwa wakisaka jumla ya pointi  15 kwenye mechi hizo za ligi, waliweza kusepa na jumla ya pointi 13 na kuyeyeyusha pointi mbili kwa kuwa walilazimisha sare mbele ya Azam FC.

Mwendo wao ulikuwa namna hii:- Simba 4-0 Ihefu, Dodoma Jiji 1-2 Simba, Simba 2-2 Azam FC, Biashara United 0-1 Simba, Simba 3-0 JKT Tanzania.

Cedric Kaze, Kocha Mkuu wa Yanga ameliambia Spoti Xtra kuwa katika hilo hana wa kumlaumu zaidi ya kufanyia kazi makosa ambayo wameyafanya.

Didier Gomes, Kocha Mkuu wa Simba ameliambia Spoti Xtra kuwa amekuwa akiwaambia wachezaji wao jukumu lao ni kutafuta ushindi ndani ya uwanja.

SOMA NA HII  SAFARI YA FEI TOTO DUBAI...SIRI IMEVUJA...TAJIRI ALIYEMSAFIRISHA HUYU HAPA...