CAF

NAMUNGO WATAJA KINACHOWAFELISHA KIMATAIFA

admin April 6, 2021 4:47 am

 


HEMED Morocco, Kocha Mkuu wa Namungo FC amesema kuwa amekuwa akishindwa kupata matokeo chanya kwa kukosa wachezaji wenye uzoefu katika mashindano ya kimataifa.

Namungo FC inawakilisha Tanzania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho ikiwa hatua ya makundi na ipo kundi D.

Ikiwa imecheza mechi tatu imepoteza mechi zote na haijaambulia pointi ambapo ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Pyramids na mabao 2-0 dhidi ya Raja Casablanca na mchezo wake wa tatu ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Nkana.

Morocco amesema:”Nimeona kwamba wachezaji wanajitahidi kusaka ushindi ila wanashindwa kutokana na wengi kutokuwa na uzoefu katika mashindano haya makubwa.

“Bado tuna mechi na tuna nafasi ya kufanyia kazi makosa ambayo tunayafanya hivyo mashabiki waendelee kutupa sapoti,”.

MAJINA MAWILI YA NYOTA WA SIMBA YAPENYA CAF GUNDOGAN: HAVERTS NI MCHEZAJI BORA ANA VITU VYA KIPEKEE

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply