Yanga SC

UONGOZI WA YANGA KUKETI NA NTIBANZOKIZA ILI KUJUA TATIZO LIPO WAPI

admin April 21, 2021 9:48 pm


 UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kuwa utakaa na mchezaji wao Said Ntobanzokiza ili kujua ni kipi ambacho kinamsumbua kutokana na kitendo chake cha kuonekana amekasirika baada ya kufunga bao, Aprili 20 mbele ya Gwambina FC.

Habari kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa nyota huyo hakupenda kuanzia benchi kwa kuwa anaamini kwaba ana uwezo mkubwa wa kucheza jambo ambalo limekuwa likiwakasirisha wachezaji wengine.

 Wakati Yanga ikishinda mabao 3-1 dhidi ya Gwambina, Ntibanzokiza alianzia benchi na aliingia kipindi cha pili akichukua nafasi ya Tuisila Kisinda ambaye aliumia.

Mshauri wa Yanga kuelekea kwenye masuala ya mabadiliko, Senzo Mbatha amesema kuwa kwa kitendo ambacho amekifanya ni lazima wazungumze naye ili kujua tatizo.

“Ikiwa mchezaji amefunga ameshindwa kushangilia hiyo inatokea kwenye mchezo kwani kila kitu kinawezekana na muda mwingine inategemea mazingira hivyo sio jambo la kuhoji sana.

“Lakini kwa kuwa imekuwa hivyo na imetokea lazima tuzungumze na mchezaji ili tujue nini ambacho kinamsumbua na tukijua nina amini kwamba tutayamaliza ila ninachojua mimi hakuna tatizo,” amesema.

GOMES: NINAIJENGA SIMBA YA MISIMU MINNE IJAYO SERIKALI YAITAKA YANGA, NAMUNGO KUIGA MFANO WA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply