Home Yanga SC YANGA YAKWEA PIPA KUWAFUATA TANZANIA PRISONS

YANGA YAKWEA PIPA KUWAFUATA TANZANIA PRISONS


 KIKOSI cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nassreddine Nabi leo Aprili 27 kimekwea pipa kuwafuata wapinzani wao Tanzania Prisons, Rukwa,Songea.

Yanga ina kibarua cha kusaka ushindi kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali na ikiwa itashinda inatinga hatua ya nusu fainali ikipoteza itakuwa haina nafasi ya kusonga mbele. 

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Aprili 30, Uwanja wa Nelson Mandela na mabingwa watetezi wa taji hilo ni watani zao wa jadi Simba.

Nahodha Msaidizi wa Yanga, Haruna Niyonzima amesema kuwa wana nafasi ya kupata ushindi kwenye mechi ambazo zimebaki na watapambana kufanya vizuri.


SOMA NA HII  VIGOGO WA SOKA AFRIKA...WAIOGOPA MECHI SIMBA NA YANGA...WAPATA VIGUGUMIZI