Simba SC

MASHABIKI WARUHUSIWA KUINGIA SIMBA V KAIZERS CHIEFS, SIMBA KUOMBA WENGINE ZAIDI

admin May 19, 2021 3:47 pm


 KUELEKEA kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kuchezwa Mei 22, Uwanja wa Mkapa, mashabiki wameruhisiwa kuingia ila watafanya maombi mengine ili kuruhusiwa mashabiki wengi zaidi.

Hii inatokana na kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona ambavyo bado vinaisumbua dunia kwa sasa.

Ni Simba v Kaizer Chiefs unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa ambapo ule wa awali wakati Simba ikikubali kichapo cha mabao 4-0 hakukuwa na mashabiki ambao waliruhusiwa kuingia katika mchezo huo.

Sasa Mei 22 uongozi wa Simba umesema kuwa umeruhusiwa kuingiza mashabiki ambao wamepata nafasi ya kuingia kwenye mchezo huo.

Haji Manara amesema:”Mpaka sasa tumeruhusiwa mashabiki 10,000 lakini tunaendelea kuomba kuongeza. Naomba uwanjani rangi iwe nyekundu na nyeupe,” .


JKT TANZANIA YAYEYUSHA POINTI TATU MAZIMA MBELE YA YANGA USIPANGE KUKOSA NAKALA YAKO JERO TU GAZETI LA SPOTI XTRA ALHAMISI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply