Simba SC

NYOTA HUYU WA MABAO AINGIA ANGA ZA SIMBA

admin May 24, 2021 7:47 am


 IMEELEZWA kuwa mtambo wa kutengeneza mabao ndani ya Kagera Sugar, David Luhende yupo kwenye hesabu za kutua Simba msimu ujao.

Habari zimeeleza kuwa nyota huyo amekuwa kwenye uangalizi mkubwa na watu wa Simba ambao wanahitaji kumnasa pale msimu utakapomeguka 2020/21.

Ndani ya Kagera Sugar, Luhende ameweka rekodi ya kucheza jumla ya mechi 30 na ametoa pasi 7 za mabao akitupia mabao mawili yote kwa mapigo huru.

Aliwatungua Azam FC akiwa nje ya 18 na aliwatungua pia Mwadui FC nje ya 18 ikiwa ni mapigo huru.

“Luhende yupo kwenye hesabu za kutua Simba hivyo kwa wachezaji wazawa chaguo namba moja ni yeye ikiwa kutakuwa na mabadiliko itakuwa kidogo sana,” ilieleza taarifa hiyo.

MANCHESTER CITY YATEMBEZA 5G IKISEPA NA KOMBE GWAMBINA FC KUENDELEA NA MAZOEZI KWA SASA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply