epl

RATIBA YA LIGI KUU ENGLAND YAWEKWA WAZI, CITY KUANZIA UGENINI

admin June 16, 2021 2:47 pm


 CHAMA cha Soka England (FA), kimetangaza ratiba ya Premier League kwa msimu wa 2021/22 ambapo tayari kila timu zishajua namna mambo yatakavyokuwa.

Msimu ujao mechi zinatarajiwa kuaza kuchezwa Agosti 14, 2021.


Katika ratiba hiyo, mabingwa watetezi, Manchester City watakuwa wageni wa Tottenham, mchezo unaotarajiwa kuwa mkali kutokana na ukubwa wa timu hizo.

Wageni ndani ya ligi hiyo, Brentford watawaalika Arsenal, huku Norwich nao wakiwa wenyeji wa Liverpool na Watford dhidi ya Aston Villa.

Mechi zingine ni; Burnley v Brighton, Chelsea v Crystal Palace, Everton v Southampton, Leicester v Wolves, Man Utd v Leeds na Newcastle v West Ham.

KEPA WA CHELSEA KUIBUKIA LAZIO KWA MKOPO YANGA: TUMEJIANDAA NA MCHEZO WETU DHIDI YA RUVU SHOOTING

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply